Mpanzu atua msimbazi, Ahmed Ally atoa kauli hii - EDUSPORTSTZ

Latest

Mpanzu atua msimbazi, Ahmed Ally atoa kauli hii

Mpanzu atua msimbazi, Ahmed Ally atoa kauli hii
Usikose kuitazama mechi ya SIMBA vs AL AHLI TRIPOLI Live bure kwenye simu yako download app yetu itakayo kuwezesha kuitazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utweza kutazama chanel za AZAM TV na DSTV bure kabisa pia na mechi zote za Nbc premier league na mechi zote za Ulaya kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA


 Winga wa zamani wa AS Vita Club Elie Mpanzu yuko nchini kukamilisha taratibu za usajili wake na Simba, imefahamika

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amethibitisha kuwa Mpanzu yuko nchini ambapo amebainisha iwapo Simba itakamilisha usajili wake basi watakuwa wameongeza ubora kwa washambuliaji wanaotokea pembeni

"Mpanzu ni mchezaji hatari na mimi nimesikia tayari yuko jijini Dar es salaam. tunao wachezaji wazuri wa pembeni kina Edwin Mbalua, Kibu Denis, Ladack Chasambi na Joshua Mutale"

"Siku hizi pembeni kuna mchango mkubwa wa mafanikio ya kupata magoli kwa hiyo niseme wazi wachezaji wanayo nafasi ya kuboresha kiwango chao ili mwalimu awe na Imani kubwa nao"

"Kama ikitokea Tumemsajili Mpanzu basi litakuwa jambo zuri kwasababu hao vijana wote niliyokutajia bado kwa namna yake wanahitaji uzoefu kwa wakongwe kama Mpanzu," alisema Ahmed

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba imebainisha kuwa Rais wa heshima Bilionea Mohammed Dewji 'Mo' ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ndye aliyefanikisha ujio wa Mpanzu ambapo atakamilisha usajili wake kisha ataanza kufanya mazoezi na kikosi cha Simba akisubiri dirisha dogo la usajili kufunguliwa ili asajiliwe rasmi katika mfumo

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz