Kuelekea mechi ya Kesho KEN GOLD vs YANGA hiki ndo alichokisema Gamondi leo - EDUSPORTSTZ

Latest

Kuelekea mechi ya Kesho KEN GOLD vs YANGA hiki ndo alichokisema Gamondi leo

Kuelekea mechi ya Kesho KEN GOLD vs YANGA hiki ndo alichokisema Gamondi leo
Usikose kuitazama mechi ya YANGA vs KEN GOLD Live bure kwenye simu yako download app yetu itakayo kuwezesha kuitazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utweza kutazama chanel za AZAM TV na DSTV bure kabisa pia na mechi zote za Nbc premier league na mechi zote za Ulaya kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA  



 Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema watahakikisha wanapambana katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ken Gold hapo kesho ili kupata ushindi utakaoendelea kuweka vyema malengo yao katika mbio za ubingwa msimu huu

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mapema leo, Gamondi alisema anatambua mchezo huo utakuwa mgumu kwa sababu kila timu inayocheza na Yanga hujipanga kusaka matokeo mazuri dhidi yao

Hata hivyo amesema ubora wa kikosi chake unampa matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo utakaopigwa uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya

"Ni mchezo wetu wa pili kwenye ligi kuu, bado kuna safari ndefu lakini huu ni mchezo muhimu kwetu na tunahitaji kupata matokeo. Leo jioni kwenye mazoezi ya mwisho nitaona Uwanja kama utaturuhusu kucheza mchezo wetu basi itakuwa nzuri kwa upande wetu na kama itakuwa tofauti tutahakikisha tunapambana kupata ushindi"

"Siku zote timu yoyote ikicheza na Yanga wanakuwa makini na kutafuta matokeo kama sisi, tutacheza kwa tahadhari na tuna wachezaji wazuri wenye uzoefu wa kucheza kwenye mazingira yoyote"

"Najua mashabiki wetu wanapenda tushinde magoli mengi, lakini sisi kama walimu tunaangalia sana kwenye uhalisia na kitu cha muhimu kwetu ni ushindi na kama mechi itaturuhusu tupate magoli mengi basi tunajituma mpaka mwisho kufanya hivyo, "alisema Gamondi

Kikosi cha Yanga kilitua mkoani Mbeya jana na leo watafanya mazoezi yao ya mwisho katika uwanja wa Sokoine

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz