Gamondi atema nyongo wanaobeza ushindi wa 1-0 - EDUSPORTSTZ

Latest

Gamondi atema nyongo wanaobeza ushindi wa 1-0

Gamondi atema nyongo  wanaobeza ushindi wa 1-0

Usikose kuitazama mechi ya YANGA vs PAMBA JIJI Live bure kwenye simu yako download app yetu itakayo kuwezesha kuitazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utweza kutazama chanel za AZAM TV na DSTV bure kabisa pia na mechi zote za Nbc premier league na mechi zote za Ulaya kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

 Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesisitiza jambo muhimu kwa kikosi chake ni alama tatu kwani sio kila mechi watafunga idadi kubwa ya mabao

Yanga iliichapa KMC bao 1-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopgwa uwanja wa Azam Complex, ukiwa ni ushindi wa pili mfululizo Yanga ikifunga bao bao moja

Akizungumza baada ya mchezo huo Gamondi aliwapongeza wachezaji wake kwa ari kubwa walioingia nayo katika mchezo huo lakini pia hakusita kuwapongeza wapinzani wake KMC kwani walikuwa madhubuti katika kujilinda

"Mimi nimefurahi kwa sababu tumeshinda, muhimu ilikuwa alama tatu. Wachezaji walicheza vizuri tulitengeneza nafasi nyingi kuliko wapinzani wetu"

"Nawapongeza KMC pia, walikuwa na nidhamu kubwa katika kujilinda, kipa wao amefanya kazi nzuri"

"Alama tatu ndio jambo muhimu kwetu, tungeweza kufunga mabao mawili au hata matatu lakini nafikiri kipa wa KMC alikuwa na siku nzuri sana leo (jana)"

"Kwangu mimi sio tatizo kushinda bao moja, inanishangaza Yanga inaposhinda bao moja mnasema lakini timu nyingine zikishinda moja mbona hamzungumzi?. Ni timu ngapi zimeshinda bao moja kwenye ligi msimu huu?", alihoji Gamondi 

Mchezo unaofuata kwa Yanga ni dhidi ya Pamba Jiji na utapigwa Alhamisi, Oktoba 03 katika uwanja wa Azam Complex

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz