Gamondi amepata dawa ya wanaopaki basi - EDUSPORTSTZ

Latest

Gamondi amepata dawa ya wanaopaki basi

Gamondi amepata dawa ya wanaopaki basi


Usikose kuitazama mechi ya YANGA vs KMC Live bure kwenye simu yako download app yetu itakayo kuwezesha kuitazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utweza kutazama chanel za AZAM TV na DSTV bure kabisa pia na mechi zote za Nbc premier league na mechi zote za Ulaya kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA


 Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amelazimika kurudi katika uwanja wa mazoezi ili kuboresha mbinu zake ili kukabiliana na timu 'zinazopaki basi'

Juzi baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KenGold, maafisa wa timu hiyo walionekana kufurahia kufungwa bao 1 tu na kumpongeza kocha wao kwa mbinu zilizowasaidia kupunguza idadi ya mabao

Katika moja ya mahojiano yake, Gamondi alisema anafahamu kila timu watakayokutana nayo kwenye ligi msimu huu, itaweka watu wengi nyuma kutafuta sare au kupunguza idadi ya mabao kwani kufungwa mabao machache na Yanga kwa wengine ni mafanikio

"Ni lazima tujipange upya ili kuwa na machaguo ya mbinu za kutengeneza mabao hata kama tunakutana na timu zinazokaa nyuma"

"Kwenye mazoezi yetu tumeanza kujipanga na hilo kuhakikisha tunakuwa tayari kukabiliana na ugumu wa namna hiyo"

"Mabeki wa pembeni, viungo na hata washambuliaji wanapaswa kuwa na njia nyingi za kutengeneza nafasi na hata kutumia nafasi ambazo watakazopata," alisema Gamondi 

Yanga imedhamiria kutetea ubingwa wake kwa msimu wa nne mfululizo, inahitaji kukusanya alama nyingi na kufunga mabao mengi

Katika mechi mbili za kwanza Yanga imeshinda zote na kufunga mabao matatu, ikiwa nafasi ya 7 katika msimamo

Wananchi wana deni la mabao sita dhidi ya watani zao Simba ambao wamefunga mabao 9 katika mechi tatu

Kazi ya kusaka pointi na mabao inaanza Jumapili hii ya kufosi katika mchezo dhidi ya KMC

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz