Yanga yashinda kesi dhidi ya Mzee Magoma - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga yashinda kesi dhidi ya Mzee Magoma

Yanga yashinda kesi dhidi ya Mzee Magoma

Usikose kuitazama Fainali ya ngao ya Jamii kati ya YANGA vs AZAM FC Live bure kupitia simu yako download app yetu kutazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utaweza kutazama chanel za Azam Tv na Dstv live bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

Yanga yashinda kesi dhidi ya Mzee Magoma

Leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikiwa ni siku ya hukumu katika kesi ya Yanga na Juma Ally Magoma ikumbukwe kwamba siku ya Jumatano ndiyo ilipangwa kesi hiyo kutolewa hukumu lakini wakili wa Mzee Juma Ally Magoma na Geofrey Mwaipopo hakutokea mahakamani na kufanya kesi kuahirishwa hadi siku ya ijumaa tarehe 9 August 2024.

Mzee Magoma na wenzake walishinda kesi waliyokuwa wamefungua mahakamni hapo wakipinga uhalali wa Baraza la Wadhamini la Yanga.

Mkurugenzi wa Sheria na Wanachama wa Simba, Wakili Simon Patrick amesema; “Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imekubaliana na hoja nne kati ya tatu ambazo Klabu ya Yanga tulizileta ili zifanyiwe marejeo.

“Kwanza mahakama ya Kisutu imekiri kwamba ni kweli haikuwa na mamlaka na kusikiliza hili shauri. Kwa mujibu wa sheria namba 318 ya mwaka 2002, masuala yote yanayohusu uhalali wa Baraza la Wadhamini yanasikiliza na Mahakama Kuu ya Tanzania.

“Kesi ya akina Magoma ililetwa hapa na ikasikilizwa na mahakama ya Kisutu, hilo lilikuwa kosa la kisheria na kupelekea mahakama ya Kisutu kukubaliana na hoja ya kwanza na kuipiga chini hukumu ya mwanzo.

“Hoja ya pili ambayo imekataliwa na mahakama ya Kisutu ni ile ya kwamba Magoma hakuwa mwanachama halali wakati akifungua shauri hilo. Mahakama imesema suala la uhalali wa uanachama linahitaji ushahidi, kwa hiyo haitasikilizwa.

“Hoja ya tatu ambayo imekubaliwa ni kwamba Mama fatuma Karume (Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini Yanga) na mzee Jabiri Katundu kwa njia za ujanja ujanja walinyimwa nafasi ya kusikilizwa.

“Watu walijitokeza mahakamani kuwawakilisha mama Karume na mzee Katundu, mahakama imechunguza kwenye rekodi na kujiridhisha kuwa watu hao hawakuwa na mamlaka kisheria kuwawakilisha mama Karume na Katundu na kupelekea mahakama kuifutilia mbali hiyo hukumu.

“Hoja ya nne ni technique kidogo, hawa watu walileta mamombi yao kwa njia ya petition wakati yalitakiwa yaletwe kama plaint, kwa kuzingatia hoja hizo mahakama ikajiridhisha na kulifutilia mbali shauri hilo.

“Hukumu hiyo imefuta na kwa vile Yanga imetumia gharama kuja hapa mahakamani, kutafuta wanasheria wa kutuaidia, mimi mwenyewe natakiwa nilipwe, nilikuwa na mawakili wengine wa Yanga, mama Karume alikuwa na wakili wake, mzee Katundu alikuwa na wakili wake, hivyo Mzee Magoma na wenzake wamemariwa kutulipa gharama za usumbufu ambazo tukikaa tukapiga hesabu vizuri zitakuwa kama tsh milioni 70 mpaka sh milioni 100," amesema Wakili Simon.

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz