Simba vs Fountain Gate bado hatihati kuchezwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba vs Fountain Gate bado hatihati kuchezwa

Simba vs Fountain Gate bado hatihati kuchezwa

Usikose kuitazama mechi ya YANGA vs VITALO FC kesho live bure kupitia simu yako download app yetu itakayokuwezesha kuitazama mechi hii live bure pia ndani ya app yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na DSTV bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

Simba vs Fountain Gate bado hatihati kuchezwa

Kikosi cha Fountain Gate kimeanza safari ya kutoka Lindi kuja jijini Dar es Salaam kwa mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba utakaopigwa Jumapili, huku ikiwa bado haijajua hatma kama mechi hiyo itachezwa au la.

Timu hiyo ilishindwa kucheza mchezo wa kwanza dhidi ya Namungo, Agosti 17 kwenye Uwanja wa Majaliwa Ruangwa, Lindi kwa sababu ya kutokamilisha taratibu za uhamisho wa wachezaji kutokana na kikosi hicho kufungiwa kutosajili.

Fountain ilifungiwa kusajili na Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa) wakati huo ikiitwa Singida FG kutokana na baadhi ya wachezaji kuidai akiwemo aliyekuwa nyota kutoka Mbrazili, Rodrigo Figueiredo Calvalho.

Hata hivyo, uongozi wa Fountain chini ya ofisa mtendaji mkuu (CEO), Kidawawa Tabitha amesema, kila kitu wameshakamilisha kwa ajili ya kumlipa mchezaji huyo na kilichobaki ni Mbrazili huyo kuthibitisha kupokea fedha hizo ili waruhusiwe rasmi.

"Ni kweli tumeshalipa kila kitu na sasa tunachosubiria ni mchezaji au wakala wake kuthibitisha pesa tuliyomtumia ili FIFA watufungulie, tunashukuru mamlaka ya soka hapa nchini wanalitambua hili na wako bega kwa bega na sisi," amesema.

Kidawawa ameongeza, uhamisho wa wachezaji wote walikamilisha kwa wakati na kuingiza katika mfumo hivyo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), linatambua hilo, na ndio maana wamekuwa karibu nao ili kumaliza changamoto hiyo inayoendelea kwao.

Akizungumzia suala hilo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Almasi Kasongo amesema, hakuna taarifa mpya ila wao kwa kushirikiana na TFF watavuta subra ili jambo hili limalizike kwa wakati kwa sababu hawataki kuvuruga ratiba ya Ligi.

"Lengo letu ni kuhakikisha ratiba tuliyoitoa inaisha kwa wakati japo tunatambua tumeanza na changamoto hii ila ni imani yetu kila kitu kitaenda kama tulivyokipanga, kwa sasa tunaendelea kuvuta subra ili tuone kile kitakachojitokeza mbele."

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz