Mzee Magoma kuilipa Yanga sh milioni 100, akishindwa kifungo kinamfuata - EDUSPORTSTZ

Latest

Mzee Magoma kuilipa Yanga sh milioni 100, akishindwa kifungo kinamfuata

Mzee Magoma kuilipa Yanga sh milioni 100, akishindwa kifungo kinamfuata

Usikose kuitazama Fainali ya ngao ya Jamii kati ya YANGA vs AZAM FC Live bure kupitia simu yako download app yetu kutazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utaweza kutazama chanel za Azam Tv na Dstv live bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

Mzee Magoma kuilipa Yanga sh milioni 100, akishindwa kifungo kinamfuata

Leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikiwa ni siku ya hukumu katika kesi ya Yanga na Juma Ally Magoma ikumbukwe kwamba siku ya Jumatano ndiyo ilipangwa kesi hiyo kutolewa hukumu lakini wakili wa Mzee Juma Ally Magoma na Geofrey Mwaipopo hakutokea mahakamani na kufanya kesi kuahirishwa hadi siku ya ijumaa tarehe 9 August 2024.

Mzee Magoma na wenzake walishinda kesi waliyokuwa wamefungua mahakamni hapo wakipinga uhalali wa Baraza la Wadhamini la Yanga.

“Hukumu hiyo imefuta na kwa vile Yanga imetumia gharama kuja hapa mahakamani, kutafuta wanasheria wa kutuaidia, mimi mwenyewe natakiwa nilipwe, nilikuwa na mawakili wengine wa Yanga, mama Karume alikuwa na wakili wake, mzee Katundu alikuwa na wakili wake, hivyo Mzee Magoma na wenzake wamemariwa kutulipa gharama za usumbufu ambazo tukikaa tukapiga hesabu vizuri zitakuwa kama tsh milioni 70 mpaka sh milioni 100.

“Mashabiki waendelee kuisapoti timu yao, ile sintofahamu ya kina mzee magoma na wenzake imefutwa rasmi leo na hawana chao tena. Sisi kwa upande wetu tumemaliza hapa kinachofuata ni kufungua kesi kudai fidia ya gharama zetu ambazo tumezitumia.

“Ni haki yao kukata rufaa lakini sheria namba 318 inasema masuala yote yanayohoji uhalali wa baraza la wadhamini yanatakiwa yapelekwe mahakama kuu, sasa wewe umepeleka mahakama ya Kisutu na Mahakama ya Kisutu imejiridhisha kuwa haikupaswa kusikiliza kesi hiyo, sasa wewe unakata rufaa kwenda wapi? Wakikata rufaa watapoteza muda ila popote waende tutawafuata.

“Unaposema gharama lazima udhithibitishe, tukikamilisha tutakwenda mahakamani kuzidai na wakishaamua mahakama kwamba anatakiwa alipe kiasi gani basi ni lazima azilipe ndani ya siku 60, akishindwa kulipa sisi kama yanga SC tutakwenda kukamata mali zake ili kufidia gharama zetu, na ikithibitika hana mali ambazo zinaweza kukidhi gharama zetu basi tutamuomba awe mfungwa “Civil Prison” mpaka atakapomaliza kulipa madeni yetu," amesema Wakili Simon.

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz