Alichokisema Ahmed Ally baada ya Yanga kuwafumua simba kwa mara ya Tatu mfululizo - EDUSPORTSTZ

Latest

Alichokisema Ahmed Ally baada ya Yanga kuwafumua simba kwa mara ya Tatu mfululizo

Alichokisema Ahmed Ally baada ya Yanga kuwafumua simba kwa mara ya Tatu mfululizo

Usikose kuitazama Fainali ya ngao ya Jamii kati ya YANGA vs AZAM FC Live bure kupitia simu yako download app yetu kutazama mechi hii bure kabisa pia ukiwa na app yetu utaweza kutazama chanel za Azam Tv na Dstv live bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

Simba vs Yanga

Meneja habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa licha ya kufungwa na watani zao Yanga SC, lakini wana kikosi kizuri ambacho wana uhakika kitafanya vizuri msimu huu.

Ahmed amesema hayo baada ya Simba kufungwa bao 1-0 na Yanga kwenye nusu fainali ya Ngao ya Jamii, mchezo uliopigwa katika Dimba la Mkapa.

"Asante Mungu. Ni matokeo mabaya lakini yenye kutupa maono wapi tunaelekea kwenye ujenzi wa kikosi chetu bora msimu huu.

"Tunakila sababu ya kujivunia maendeleo ya project yetu ya muda mrefu iliyohusisha wachezaji wengi wapya wenye vipaji vikubwa na umri mdogo.

"Wana Simba SC matokeo ya leo yasiwatie unyonge kwani tupo katika njia sahihi sana na punde tutaanza kuogelea kwenye mito ya asali.

"Hii ni tofauti na msimu uliopita tulichukua ngao ya jamii lakini hatukua na timu imara ndio maana tukakosa Makombe yote, Msimu huu tumekosa Ngao lakini tunayo timu imara ya kutupa heshima hapo baadae.

"Muda sio Mrefu tu ,Maji yatajitenga na mafuta, muda si mrefu. Memkwa utawaona Muda si Mrefu ngoja tu Ligi ichanganye. Mimi Timu ninayo.

"Mimi Kwa mara yakwanza tangu Nimeanza kazi Simba sijawahi kuona Mashabiki Wanawashangilia Wachezaji huku Timu imepoteza tena umefungwa na Mpinzani wako Namba Moja alafu watu wanashangilia we huoni kama ni Ubaya Ubwela huo.

"Hii Simba sio ya kawaida, hii Simba itakuja Kufanya balaa kubwa mno, hii Simba ni ya kiwango cha hali ya juu mno," amesema Ahmed Ally.

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz