Alicho kisema Skudu baada ya kupewa mkono wa kwaheri na Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

Alicho kisema Skudu baada ya kupewa mkono wa kwaheri na Yanga

Alicho kisema Skudu baada ya kupewa mkono wa kwaheri na Yanga

Usikose kuitazama mechi ya KAGERA SUGAR vs YANGA live bure kupitia simu yako download app yetu itakayokuwezesha kuitazama mechi hii live bure pia ndani ya app yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na DSTV bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA


 Baada ya msimu mmoja wa mafanikio akiwa na Yanga, winga Skudu Makudubela amewaaga rasmi Wananchi baada ya mkataba wake kumalizika

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Skudu ameishukuru familia ya Yanga kwa nyakati mzuri alizopata katika kipindi chote alichokuwa hapa nchini

"Ninaandika ili kutoa shukrani zangu za dhati kwa Familia nzima ya Yanga kwa upendo mlioonyesha kwangu wakati nikiwa Tanzania"

"Fadhilia na uchangamfu wenu umeacha alama isiyofutika moyoni mwangu. Kwa uongozi wa klabu, hasa Bw. GSM na Rais Bw. Hersi, natanguliza shukrani zangu za dhati kwa imani mliyoonyesha kwangu. Imani yenu imemaanisha ulimwengu kwangu"

"Ni heshima iliyoje kuiwakilisha Taasisi adhimu kama hii. Benchi la ufundi, linaloongozwa na Kocha Miguel Gamondi, imekuwa furaha kabisa kufanya kazi nayo. Ninashukuru kwa nafasi ya kujifunza kutoka kwako na kukua kama mchezaji"

"Kwa wachezaji wenzangu na marafiki, Nyinyi ni askari wa kweli, na nina heshima kuwa nimeshiriki mchezo nanyi. Endelea kuangaza, na Mungu awabariki nyote," aliandika Skudu

Akiwa na Yanga Skudu alifanikiwa kushinda mataji mawili, Ligi Kuu na kombe la FA huku akiwa sehemu ya kikos kilichocheza robo fainali ya ligi ya mabingwa

Kila la kheri Waziri wa raha......!

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz