Mkata Umeme Maniema aingia katika rada za Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

Mkata Umeme Maniema aingia katika rada za Yanga

Mkata Umeme Maniema aingia katika rada za Yanga
Usikose kutazama live mechi za EURO 2024 bure kwenye simu yako download app yetu kutazama pia chanel za Azam tv zote bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

 Baada ya kuachana na kiungo Zawadi Mauya, Yanga inatarajiwa kusajili kiungo mkabaji mwingine ambapo mabingwa hao wa Tanzania Bara wanahusishwa na 'mkata umeme' kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Onoya Sangana Charve (21), anayeichezea Klabu ya AS Maniema

Yanga imedhamiria kufanya vizuri hasa katika michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao hivyo inaimarisha kila idara ili kuwa na kikosi kipana mara dufu

Imeelezwa kuwa Kocha Mkuu, Miguel Gamondi, ameagiza atafutwe kiungo mkabaji mwingine mwenye uwezo kama Khalid Aucho ambaye mara nyingine anapokosekana kikosini Yanga huyumba katika eneo la kiungo

"Tumeona ni kweli, misimu miwili eneo hilo linatuponza, tulifungwa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika na USM Alger ya Algeria kwa sababu tulimkosa Aucho aliyekuwa na kadi"

"Hatukufanya vizuri dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini hatua ya robo fainali moja kati ya sababu ni kwamba hatukuwa na wachezaji wetu nyota wenye uwezo mkubwa akiwamo Aucho kwa sababu mbalimbali, na kuna wakati hapa alikuwa majeruhi, kwa hiyo lazima tupate mtu mwingine," kilisema chanzo

Yanga imekuwa na mahusiano mazuri na AS Maniema msimu uliopita ikimsajili Max Nzengeli

Mpaka sasa Yanga imehusishwa kuwawania nyota wawili wa timu hiyo Sangana na kiungo mshambuliaji Agee Basiala Amongo

JIUNGE NA GROUP LA WAKUBA HAPA 18+ HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz