Kuna Aziz Ki, Chama, Pacome na Maxi - EDUSPORTSTZ

Latest

Kuna Aziz Ki, Chama, Pacome na Maxi

Kuna Aziz Ki, Chama, Pacome na Maxi


Michuano ya EURO 2024 inaendelea pia ligi mbali mbali karibu zinaanza usikose kuzitazama mechi hizi zote LIVE bure kupitia simu yako download app yetu kutazama chanel zote za Azam tv bure pia ukiwa na app yetu utaweza kutazama muvi zilizotafsiriwa kwa kiswahili download app yetu sasa kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

 Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga jana walitangaza kumsajili kiungo mshambuliaji Clatous Chama aliyeng'olewa kutoka kwa watani zao Simba

Usajili huo ni wazi unakwenda kuongeza upana wa kikosi hasa katika eneo la viungo washambuliaji ambao sasa ni jukumu la kocha Miguel Gamondi kuamua nani aanze kwenye kikosi 

Kabla ya kusajiliwa kwa Chama, Gamondi amekuwa na nyota watatu aliowategemea zaidi kama viungo wa ushambuliaji ambao ni Max Nzengeli, Aziz Ki na Pacome Zouzoua ambao msimu uliopita walifunga jumla ya mabao 39

Usajili huo wa Chama ndani ya Yanga sasa utamfanya kocha Gamondi kuwa na machaguo mengi zaidi katika eneo hilo ingawa Mzambia huyo pia ana uwezo wa kucheza kama mshambuliaji anayetokea pembeni kama ilivyo kwa Pacome na Maxi

Katika msimu wake wa mwisho na Simba, Chama alipachika mabao saba na pia akitokea assist 7

Chama amejiunga na Yanga baada ya tetesi za muda mrefu, Mzambia huyo alimaliza mkataba wake wa kuichezea Simba Juni 30, mwaka huu

Haikuwa rahisi kwake kufikia uamuzi wa kujiunga na Yanga kwani klabu yake ya zamani Simba walikuwa tayari kumbakisha kwa gharama yoyote

Hadi mapema jana alipotambulishwa, viongozi wa Simba walikuwa bado wanahaha wakijaribu kumshawishi asitishe mpango wa kutua Jangwani



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz