Kibu haidai Simba - Ahmed - EDUSPORTSTZ

Latest

Kibu haidai Simba - Ahmed

Kibu haidai Simba - Ahmed


Usikose kuitazama mechi ya YANGA vs TS GALAXY FC michuano ya Mpumalanga cup Live hapa bure

Ni kesho saa 10: 0 jioni usikose kuitazama mechi hii LIVE bure kupitia simu yako download app yetu mapema ili uweze kuitazama mechi hii kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA


 Meneja wa Habari na Mwasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema kiungo mshambuliaji Kibu Denis amelipwa fedha zake zote za usajili na ndio maana aliongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Simba

Ahmed amesema uongozi unashughulikia suala lake ili ajiunge na wenzake Misri lakini mpaka sasa hajatuma hati yake ya kusafiria kama alivyoagizwa

"Simba tayari imeshamlipa Kibu Denis pesa zake zote na amesaini mkataba wa miaka 2 na Klabu yetu. Hakuna anachotudai kwa sasa ndiyo maana tunashughulikia uwezekano wa mchezaji kujiunga na wenzake kambini Misri

"Kwa taarifa niliyokuwa nayo tayari tumeshamwambia atutumie passport yake ili tuweze kufanya tratibu za kumkatia Visa ili aweze kujiunga na wenzake kambini huko Misri ila mpaka sasa bado hajatutumia," alisema Ahmed

Wakati Ahmed akitoa taarifa hiyo, kuna kila dalili huenda Kibu asisafiri kwenda Misri badala yake akaungana na timu pale itakaporejea nchini

Simba iko katika wiki ya mwisho la pre-season ambapo Kocha Mkuu Fadlu Davis jana alisema wako katika program za kuhitimisha kambi yao hapo Misri na pengine huenda Simba ikarejea nchini mwishoni mwa wiki

Kwa muda uliobaki Kibu anaweza kufanya mazoezi ya siku mbili tu au tatu jambo ambalo naamini Simba haiwezi kutumia gharama kumsafirisha Misri kwa ajili ya mazoezi ya siku mbili

Lakini pia kuna taarifa kutoka ndani ya uongozi kuwa Kibu atakatwa mshahara kwa kitendo cha kushindwa kushiriki pre-season na wenzake huku taarifa za ndani zikidokeza kuwa Kibu amepata ofa kutoka klabu moja kubwa Norway ambapo yuko kwenye mvutano na uongozi akishinikiza kuvunja mkataba wake

Suala lake linataka kufanana na lile la Coastal Union kuhusu Lameck Lawi ambaye tayari yuko Ubelgiji kukamilisha taratibu za kujiunga na KRC Genk

Coastal Union walipata ofa hiyo wakiwa tayari wako kwenye mchakato wa kumuuza Lawi Simba na ghafla kuamua kusitisha mazungumzo na Simba pamoja na kurejesha fedha walizokuwa tayari wamepokea kutoka kwa Simba

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz