Kamwe amaliza mkataba Yanga, Awaaga mashabiki - EDUSPORTSTZ

Latest

Kamwe amaliza mkataba Yanga, Awaaga mashabiki

Kamwe amaliza mkataba Yanga, Awaaga mashabiki
Ni kesho kutwa SIMBA DAY usikose kutazama sherehe hii LIVE bure kupitia simu yako download app yetu mapema ili uweze kuitazama na mechi ya kirafiki itakayo chezwa siku hiyo kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

 Meneja wa Kitengo cha habari na Mawasilino wa Yanga Ali Kamwe amewaaga mashabiki na wanachama wa timu hiyo baada ya mkataba wake kumalizika

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, jana usiku Kamwe aiiweka chapisho la kuwaaga Wananchi baada ya utumishi adhimu wa miaka miwili

"A Good dancer must know when to Leave a Stage. Mtumbuizaji mzuri anatakiwa kujua ni wakati gani wa kuondoka jukwaani"

"Maneno ya hekima kutoka katika kinywa cha Patrick Loch Otieno Lumumba; Na ni Hekima hii, inanituma mbele yenu Wananchi, Mashabiki na Wanachama wa Klabu yetu pendwa, kuwaambia kuwa, Ni wakati sasa wa kijana wenu kuondoka Jukwaani"

"Nimesimama Miaka miwili juu ya hili Jukwaa, Tumeimba, Tumecheza, Tumefurahi na Alhamdulillah Tumeshinda pamoja kila pambano Lililokuja mbele yetu"

"Muda wangu umemalizika na Asanteni sana. Tutaonana tena Wakati mwingine nikiwa na kitu kizuri cha kuwaonyesha Juu ya Jukwaa," aliandika Kamwe

Kamwe alitambulishwa Yanga mwaka 2022 akichukua nafasi ya Hassan Bumbuli ambaye mkataba wake ulimalizika

Hata hivyo bado Wananchi wanamuhitaji Kamwe na pengine huenda wakaendelea kuwa nae lakini akiwa na majukumu mapya

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz