Chama apagawa na 'Welcome' ya Wananchi - EDUSPORTSTZ

Latest

Chama apagawa na 'Welcome' ya Wananchi

Chama apagawa na 'Welcome' ya Wananchi


Usikose kutazama live mechi za EURO 2024 bure kwenye simu yako download app yetu kutazama pia chanel za Azam tv zote bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA


 Kiungo mshambuliaji wa Yanga Clatous Chama amewashukuru mashabiki na wanachama wa Yanga kwa ukaribisho wa aina yake

Jana Yanga ilimtambulisha Chama kwa utambulisho rasmi baada ya hapo awali kumtambulisha kupitia picha za kusaini mkataba

Chama amesema amefurahia na vile Wananchi walivyompokea na kuwaahidi kuwafanyia mambo makubwa uwanjani

"Nafurahi kujiunga na timu hii kubwa zaidi Tanzania. Nawashukuru Wananchi kwa mapokezi yao kwa kweli nimepokelewa vizuri"

"Sitazungumza mengi kwa sasa lakini nawaahidi, watafurahi uwanjani," alisema Chama

Baada ya usajili wake kutangazwa wiki iliyopita, Wananchi wakiongozwa Msemaji wa klabu Ali Kamwe waliandamana mitaani kufurahia usajili wake

Kama haitoshi likafanyika tukio maalum la kula keki Makao Makuu ya Yanga, Jangwani ambapo keki 17 zililiwa na Wananchi ikiwa ishara ya kumkaribisha Chama nayependelea kuvaa jezi namba 17

Chama tayari ameungana na kikosi cha Yanga kilichoanza maandalizi ya pre-season. Yanga inatarajiwa kuelekea Afrika Kusini wiki ijayo kwa ajili ya maandalizi ya Toyota Cup ambapo Julai 28 watachuana na Kaizer Chiefs

KUPATA KIFURUSHI CHA DATA VODA BOFYA + HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz