Yanga yaja na staili mpya ya usajili - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga yaja na staili mpya ya usajili

Yanga yaja na staili mpya ya usajili

Mechi za EURO 2024 na COPA AMERICA zinaendelea leo usikose kuzitazama mechi zote LIVE bure kwenye simu yako download app yetu uweze kuzitazama pia ukiwa na app yetu utaweza kutazama muvi zilizotafsiriwa kwa kiswahili pia utaweza kutazama chanel za azam tv na dstv bure download app yetu sasa bonyeza 👉🏻👉🏻HAPA

Yanga na staili mpya ya usajili

Klabu ya Yanga SC imekuja na staili mpya ya usajili chini ya Rais wake Injinia Hersi Said waliyoanza kuitumia ndani ya misimu hii miwili mfululizo chini ya uongozi wake imewapa makombe manne.

Timu hiyo chini ya Hersi, imeboresha kikosi chao kwa kufanya usajili wa kisasa uliowapa mafanikio ukiwemo baadhi ya Pacome Zouzoua, Yao Koaussi, Maxi Nzengeli.

Wengine ni Stephane Aziz Ki, Djigui Diarra, Kennedy Musonda na Khalid Aucho ambapo timu hiyo imetwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Bara mara tatu na Mshindi wa pili katika Kombe la Shirikisho pia kufuzu hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumza nasi, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe alisema kuwa tangu Hersi na Kamati ya Utendaji hiyo imeingia madarakani, wameingia mbinu mpya ya usajili wa wachezaji ambayo wanaifanya wakati ligi za nchi zote zinaendelea.

Kamwe alisema kuwa mbinu imewawezesha kufanya uchaguzi mzuri wa wachezaji wakati huo timu nyingine zikiwa bize na ligi wao wanakamilisha dili za usajili.


Aliongeza kuwa katika kuthibiisha hilo, wao kabla ya ligi haijamalizika usajili wao ulikamilika kwa asilimia kubwa, kilichobaki kuwatambulisha kuanzia Julai Mosi, mwaka huu.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz