Taarifa Mpya kutoka simba Asubuhi hii - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa Mpya kutoka simba Asubuhi hii

 Taarifa Mpya kutoka simba Asubuhi hii

Leo ni Yanga vs Safari champions usikose kuitazama mechi hii live bure kupitia simu yako pia mechi za Euro 2024 zinaendelea leo usikose kuzitazama live bure download app yetu itakayorusha mechi zote hizi live bure kumbuka pia ukiwa na app yetu utaweza kutazama muvi zilizotafsiriwa pia na chanel za Azam tv bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻HAPA

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amewatoa hofu wapenzi na wanachama wa klabu hiyo kuwa michakato ya usajili inaendelea na wako katika hatua za mwisho kukamilika

Baada ya kutoa Thank You kwa wachezaji watano pamoja na kutangaza usajili wa beki Lameck Lawi, ukimya umetawala Msimbazi jambo lililowapa hofu baadhi ya Wanamsimbazi wenye shauku kubwa ya kutaka kufahamu maboresho ya kikosi

"Usajili unaendelea, mpaka sasa umekamilika kwa asilimia kama 97 hivi, hivyo mashabiki wasione kama tuko kimya, tunakamilisha ujenzi wa nyumba yetu"

"Kuanzia wiki ijayo tutaanza kutangaza wachezaji wote tuliowasajili, itakuwa bandika- bandua bila ya kupumzika"

"Najua shauku ya Wanamsimbazi lakini niwahakikishie tumeleta vyuma kwelikweli. Baadhi ya wachezaji tayari wameshatua kwa ajili ya taratibu za maandalizi ya pre-season," alisema Ahmed

Simba inatarajiwa kuondoka nchini wiki ijayo kuelekea Misri kwa ajili ya pre-season itakayodumu kwa wiki tatu na kikosi kurejeea kwa ajili ya Tamasha la Simba Day litakalofanyika August 03



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz