Simba yashusha kiungo Mcongo - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba yashusha kiungo Mcongo

Simba yashusha kiungo Mcongo


Ligi mbali mbali zitaanza muda si mrefu download app yetu kutazama mechi zote za ligi kuu tanzania bara na ulaya live bure kabisa pia ndani ya app yetu utaweza kutazama muvi zilizotafsiriwa kwa kiswahili pia utaweza kutazama chanel za azam tv buree kabisa kudownload app yetu bonyeza 👉🏻👉🏻HAPA


 Klabu ya Simba inatajwa kukamilisha usajili wa kiungo kutoka Jamhuri ya Congo Debora Mavambo Fernandesn (mwenye jezi nyeupe pichani juu) aliyekuwa aakiitumikia Mutondo Stars ya Ligi Kuu Zambia (MTN)

Kiungo huyo wa kati mzaliwa wa Angola mwenye umri wa miaka 24 tayari yuko nchini na huenda akawa miongoni mwa wachezaji watakaotambulishwa na Simba siku chache zijazo

Debora ameitumikia Mutondo FC msimu mmoja akijiunga akitokea klabu ya Academica Petroleos do Lobito ya Angola mwaka 2023

Kiungo huyo anamudu kucheza eneo la kiungo mkabaji lakini pia mara chache ametumika katika safu ya ulinzi

Ujio wa Debora huenda ukashuhudia Simba ikiachana na Sadio Kanoute au Babacar Sarr

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema uongozi uko kwenye majadiliano ya kusitisha mikataba ya baadhi ya wachezaji

Taarifa za wachezaji hao kupewa 'Thank You' zitatolewa baada ya michakato hiyo kumalizika



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz