Meneja wa Mwanyeto: Ofa ya Simba iko mezani na ni nono - EDUSPORTSTZ

Latest

Meneja wa Mwanyeto: Ofa ya Simba iko mezani na ni nono

Meneja wa Mwanyeto: Ofa ya Simba iko mezani na ni nono

Mechi za EURO 2024 zinaendelea leo usikose kuzitazama mechi zote live bure kwenye simu yako download app yetu kuzitazama pia ndani ya app yetu kuna muvi zilizotafsiriwa kwa kiswahili pia zipo chanel za Azam tv na Dstv zote utazitazama bure kudownload app yetu bonyeza 👉🏻👉🏻HAPA

Bakari Mwamnyeto.

Meneja wa wa Nahodha wa Klabu ya Yanga, Bakari Mwamnyeto aitwaye Carlos Sylivester amesema kuwa wamepokea ofa ya Klabu ya Simba kutaka huduma ya mchezaji huyo.

Simba wanatajwa kuitaka huduma ya Mwamnyeto kama mbadala wa Henock Inonga Baka ambaye ametimkia AS FAR Rabat ya nchini Morocco.

“Hakuna kinachokwamisha, ni suala la muda tu, muda sahihi ukifika tutajua mustakabali. Kwa sasa mazungumzo yanaendelea vizuri na sioni kitu cha kukwamisha lakini suala la kusema tumemalizana na Yanga bado.

“Unapoongelea ofa za hizi timu mbili, kitu ambacho Simba ana ofa sidhani kama Yanga anaweza kushindwa ku-ofa ama anachoweza ku-ofa Yanga basi Simba nae anaweza ku-ofa. Kikubwa ni uatayari wa mchezaji anataka kwenda kufanya wapi kazi.

“Maongezi yanaendelea vizuri lakini kwa mtu kama Mwamnyeto ni beki mzuri, ni nahodha wa yanga na amecheza kwa mafanikio makubwa ndani ya klabu, hajapata changamoto ambayo klabu haimhitaji, kwa hiyo maamuzi yanaweza kuchukua muda kwa sababu lazima ufikirie suala la kubadilisha mazingira.


“Pia ofa ambazo zinakuja na suala la uongozi wa mchezaji kukutana na uongozi wa timu, hicho ndicho kitu ambacho kimeleta tofauti lakini mazungumzo yako sawa. “Ni kweli ofay a Simba ipo mezani na ni nzuri pia, lazima tuitafakari pia. Ni suala la muda kama nilivyosema, muda utazungumza,” amesema Carlos.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz