Huu hapa uamuzi wa simba kuhusu Juma mgunda - EDUSPORTSTZ

Latest

Huu hapa uamuzi wa simba kuhusu Juma mgunda

Huu hapa uamuzi wa simba kuhusu Juma mgunda

Ligi mbali mbali zitaanza muda si mrefu download app yetu kutazama mechi zote za ligi kuu tanzania bara na ulaya live bure kabisa pia ndani ya app yetu utaweza kutazama muvi zilizotafsiriwa kwa kiswahili pia utaweza kutazama chanel za azam tv buree kabisa kudownload app yetu bonyeza 👉🏻👉🏻HAPA

 

Kaimu Kocha Mkuu wa Simba Juma Mgunda amehakikishiwa na mabosi wa timu hiyo ataendelea kubaki katika benchi la ufundi hata ikitokea mabadiliko katika nafasi yake

Mgunda anawindwa na klabu ya Coastal Union ambayo inamuhitaji kwa ajili ya kujiimarisha kuelekea michuano ya kombe la Shirikisho msimu ujao

Wakati Simba ikiwa bado haijatangaza hatma ya benchi la ufundi, usajili unaofanyika sasa umetokana na ripoti ya makocha Abdelhak Benchikha na Mgunda ambaye ndiye aliyemaliza msimu akiwa Kocha Mkuu

Litakuwa jambo la kushangaza kama Simba itaachana na Mgunda na kuleta watu wapya katika benchi la ufundi ambao hawafahamu masuala mengi kuhusu klabu

Na pengine hii ndio sababu uongozi umeona lazima Mgunda abaki hata kama kwa nafasi ya Kocha Msaidizi ikitokea mabadiliko katika nafasi ya kocha mkuu

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema taarifa kuhusu benchi la ufundi itatolewa wakati wowote kabla ya kikosi kuelekea Misri wiki ijayo



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz