Simba walamba udhamini mpya wa bia wenye thamani ya Bil. 1.5 - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba walamba udhamini mpya wa bia wenye thamani ya Bil. 1.5

 Simba walamba udhamini mpya wa bia wenye thamani ya Bil. 1.5

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Katika kuelekea mchezo wao wa Dabi dhidi ya Yanga SC, Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wameingia mkataba wa Bil. 1.5 na Kampuni ya Serengeti Breweries kupitia bia yao ya Pilsner Lager.


Simba wametangaza udhamini huo hii leo Novemba Mosi, 2023 wakati dabi yao inakwenda kupigwa Jumapili Novemba 5, 2023.


"Tunajivunia kuziunganisha taasisi mbili kubwa za SBL na Simba kwa mkataba wa udhamini wa miaka mitatu. Kupitia udhamini huu utaifanya bia yetu ya Pilsner Lager kuwa mdhamini wa Simba."


"Udhamini huu utakuwa na thamani ya Tsh. 1.5 bilioni. Kwa udhamini huu tunaamini utasaidia kukuza michezo nchini kwetu. Simama Imara, Songa Mbele Kama Simba," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Serengeti ​Breweries Limited, Obinna Anyalebechi.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz