Robertinho awakosa watano maandalizi Super Ligi - EDUSPORTSTZ

Latest

Robertinho awakosa watano maandalizi Super Ligi

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 
Nyota watano hawapo na kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Robertinho Oliveira kutokana na kukabiliwa na majukumu ya timu za Taifa


Uongozi wa Simba ulifanya jitihada za kuomba wachezaji hao wabaki kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa African Football League dhidi ya Al Ahly ambao utapigwa Ijumaa ijayo Oktoba 20, ni wazi imeshindikana


Wachezaji hao ni Henock Inonga ambaye yupo na timu ya taifa ya DR Congo iliyoweka kambi New Zealand, Clatous Chama yupo Misri na kikosi cha timu ya taifa ya Zambia, Kibu Dennis, Mzamiru Yassin na Ally Salim hawa wapo kwenye kikosi cha Stars kilichosafiri leo UAE


Taifa Stars inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Sudan itakayochezwa Saudi Arabia Oktoba 15


Taarifa kuoka Misri zimebanisha kuwa wapinzani wa Simba Al Ahly wao wamefanikiwa kuwazuia wachezaji wao wote walioitwa timu za Taifa ili kujiandaa na mchezo dhidi ya Simba


Al Ahly wanatarajiwa kutua nchini Oktoba 17 kwa ajili ya mchezo huo



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz