Kibwana shomari afunguka Haya kuhusu Kupigwa benchi na Yao Kouassi - EDUSPORTSTZ

Latest

Kibwana shomari afunguka Haya kuhusu Kupigwa benchi na Yao Kouassi

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mlinzi wa kulia wa Yanga Kibwana Shomari amekiri kuwa mchezaji mwenzake katika nafasi hiyo Yao Kouassi anampa darasa


Tangu atue Yanga katika dirisha la usajili lililopita, Yao amejihakikishia nafasi mbele ya Kibwana ambaye katika misimu miwili iliyopita alitumika kwenye 'mbavu' zote


Kibwana amesema Yao anaonyesha uwezo mkubwa, kuna vitu vingi anafanya uwanjani ambavyo nae anaweza kuviiga ili kuwa bora zaidi


"Ni kweli sasa sipati nafasi, nakubali kuzidiwa uwezo na Yao. Ni mchezaji mzuri ambaye ana uwezo mkubwa wa kukaba na kushambulia"


"Ana pumzi akipanda anawahi kurudi kuzuia mashambulizi na ana nguvu. Hilo limeniamsha na kunipa akili ya kuongeza ujuzi zaidi ili nirudi kwenye ushindani"


"Bado nina nafasi ya kucheza na nitafanya kwa ubora ili kumpa imani kocha kuwa hakosei kunipa nafasi ya kucheza," alisema Kibwana


Yao ndio kinara kutoa pasi za mabao kwenye ligi kuu ya NBC akitoa pasi tatu huku pia akiwa amefunga bao moja



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz