Dimba la Mkapa liko tayari kwa Super Ligi - EDUSPORTSTZ

Latest

Dimba la Mkapa liko tayari kwa Super Ligi

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro amekagua maendeleo ya ukarabati ya awamu ya kwanza yanayoendelea katika Uwanja wa Mkapa jijini Dar na kusema umefikia asilimia 95 na asilimia tano zilizobaki zinatarajiwa kukamilika ndani ya siku tano kuanzia leo Oktoba 9.


Dk Ndumbaro amesema tayari vyumba vinne vya wachezaji, sehemu ya kuchezea, vyumba vya waamuzi, afya na eneo la video za marejeo (VAR) vimekamilika.


"Tayari taa za kisasa 320 za mfumo wa LED zimefungwa na kuna huduma ya mtandao wa bure kabisa kwa ajili ya watazamaji wa mechi ambao tutauzindua kati ya Oktoba 17 hadi 19 mwezi huu kabla ya mchezo wa ufunguzi wa African Football League kati ya Simba na Al Alhy Oktoba 20, 2023 " amesema Dk Ndumbaro


Ameongeza kuwa, katika eneo la watu mashuhuri (VIP) na sehemu ya wandishi wa Habari kazi iliyobakia ni ndogo ambayo itamalizika ndani ya siku hizo tano akiongeza kuwa mfumo wa sauti uwanjani tayari umerekebishwa.


Dk Ndumbaro amesema kuwa Kampuni ya Formula 360, itafunga mfumo wa matangazo kidijitali ambao utaanza kufanya kazi rasmi Oktoba 20 huku akisistiza kuwa baada ya mchezo huo, ukarabati mkubwa wa awamu ya pili utaendelea.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz