Ahmed Ally aukubali mziki wa Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

Ahmed Ally aukubali mziki wa Yanga

 Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao dhidi ya Azam FC.

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Uongozi wa Klabu ya Simba umeweka wazi kuwa utadhihirisha ukubwa wao kwa kupata ushindi kwenye mchezo wa Kariakoo Dabi dhidi ya Yanga unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa.


Ni Kariakoo Dabi inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ndani ya dakika 90 kwa timu zote kuwania kupata pointi tatu muhimu.


Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally ameweka wazi kuwa wanatambua ushindani utakuwa mkubwa na wapo tayari kwa ajili ya kupata matokeo kwenye mchezo huo.


"Azam hawezi kutufikia tena, mpinzani aliyebaki ni Yanga ambaye na yeye tunataka kumfunga na kumpita kwa alama sita. Ni mechi ambayo tunaitaka kweli kweli, kuanzia kwa mashabiki, benchi la ufundi, wachezaji na viongozi ndio hata hatulali,"


Ndivyo alivyonukuliwa Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally katika Mkutano wake na wanahabari kuelekea mchezo wao wa ‘Kariakoo Derby’ watakapomenyana dhidi ya kikosi cha Yanga kuwania ubingwa Ligi Kuu Tanzania.


"Tumewekeza zaidi kwenye kuwafurahisha mashabiki wetu, Jumapili ya Novemba 5, 2023 tunataka kuwafurahisha. Na anayeshinda mchezo huo ndio atatawala nchi hadi tukikutana tena," amesema Ahmed.


Amesema "Tumecheza mechi ngumu lakini mechi ya Jumapili ni ngumu kuliko zote hii ni kutokana na utani uliopo pamoja na ubora wa timu yao. Tunaona namna wachezaji wao wanajituma. Mechi yetu dhidi yao ni ngumu kweli kweli, mechi ya kipimo cha mpira wa nchi haiwezi kuwa nyepesi."


Aidha, kiongozi huyo amewaasa mashabiki wa klabu hiyo kijitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuwapa nguvu wachezaji wao, sambamba na hayo amewaasa kuwa watiifu kwa kuzingatia kampeni ya kuhamasisha vitendo vya kiungwana michezoni ‘Fair play’.


"Mashabiki wetu tuzingatie misingi ya uungwana na ustaarabu, tujitahidi tushangilia na kutaniana kwa heshima ili kuepusha vurugu. Tuendeleze Utanzania kwa utu na upendo," amesema Ahmed.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz