Yanga yajaza mabasi saba safari ya Rwanda - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga yajaza mabasi saba safari ya Rwanda

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Wananchi hawana jambo dogo ndivyo unavyoweza kusema baada ya mashabiki na Wanachama wa Yanga kuendelea kujiandikisha kwa ajili ya safari ya Rwanda kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Merrikh


Mpaka sasa, Yanga imethibitisha kuwa mabasi saba yamejaa baada ya mashabiki na Wanachama kulipia gharama ya safari


Kutakuwa na mabasi maalum kutoka jijini Dar es salaam ambayo gharama ni Tsh 150,000/- kwenda na kurudi ikiwa ni pamoja na tiketi ya kuingia dimba la Pele, Kigali Jumamosi Septemba 16 2023


Pia kutakuwa na mabasi kutoka mikoa ya Kigoma, Kagera na Mwanza ambapo utaratibu unaandaliwa katika Matawi ya mikoa husika


Uwanja wa Pele unachukua takribani mashabiki 22,000, Wananchi wamepania kwenda kuujaza uwanja huo


Hapo bado hujazungumzia Wananchi wa Rwanda ambao wanaisubiri kwa hamu kubwa Yanga


Safari itakuwa Alhamisi Septemba 14, bado mashabiki wanaendelea kujitokeza ambapo zoezi litafungwa Jumanne ijayo, Septemba 12


Kwa hakika huko Rwanda Yanga itakuwa kama nyumbani tu




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz