Yanga waingia kambini Leo kuiwinda El merrikh - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga waingia kambini Leo kuiwinda El merrikh

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Baada ya mapumziko ya mwishoni wa wiki, kikosi cha Yanga leo kinarejea mazoezini kuendelea na maandalizi ya mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika


Jumamosi ya Septemba 16 2023, Yanga itakuwa ugenini nchini Rwanda kumenyama na El Merrikh katika mchezo wa mkondo wa kwanza


Meneja wa Yanga Walter Harrison amesema kutakuwa na 'session' za mazoezi mfululizo yaliyoandaliwa na Kocha Miguel Gamondi na benchi lake la ufundi lengo likiwa kuhakikisha wanakuwa tayari kwa mchezo dhidi ya El Merrikh


Aidha Harrison amesema wanatarajia kucheza mechi moja ya kirafiki wiki hii ikiwa ni sehemu ya maandalizi


"Baada ya mapumziko ya mwishoni mwa wiki timu itaendelea na mazoezi Jumatatu (leo). Tutakuwa na session mbalimbali za mazoezi kwa kuzingatia mipango ya benchi la ufundi"


"Kwa muda tulionao, pengine tutacheza mechi moja ya kirafiki kabla ya timu kuelekea Rwanda tayari kwa mchezo," alisema Harrison


Habari njema kwa Gamondi ni kuwa baadhi ya wachezaji walio kwenye majukumu ya timu za Taifa watarejea mapema baada ya mechi za kuwania kufuzu michuano ya Afcon 2023


Nyota nane wa Yanga ambao wako na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' wanatarajiwa kurejea kujiunga na wenzao baada ya mchezo dhidi ya Algeria utakaopigwa Alhamisi, Septemba 07



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz