Uganda waishutumu Tanzania Kipanga MATOKEO mechi ya Afcon - EDUSPORTSTZ

Latest

Uganda waishutumu Tanzania Kipanga MATOKEO mechi ya Afcon

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 
Kocha wa Uganda, Milutin Sledjovic Micho ametoa shutuma kwa Algeria na Tanzania kuwa ni kama walipanga kutoka sare kwenye mchezo wao uliopigwa dimba la Annaba uliofanikisha Tanzania kufuzu AFCON


Micho anadai kuwa ni kama Algeria walipanga na Tanzania kufanya hivyo ili kuirahisishia Taifa Stars kufuzu na wao kuangukia pua licha ya timu yake kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Niger


Kocha huyo ameomba Algeria na Tanzania kutolea ufafanuzi suala hili na abainike aliyehusika na suala zima


Aidha aliongeza kuwa kila mmoja anatambua DNA ya kocha wa Algeria, Djamel Belmadi katika suala zima la kusaka ushindi hivyo haamini kama Tanzania walipata sare kwa uwezo


Tanzania iliungana na Algeria kufuzu michuano ya Afcon 2023 baada ya kumaliza nafasi ya pili kundi F ikiwa na alama nane


Uganda walimaliza nafasi ya tatu wakiwa na alama saba. Ni wazi malalamiko ya Micho ni baada ya timu yake kukosa nafasi lakini kwa wlaiofuatilia mchezo kati ya Algeria na Tanzania wanafahamu ni kwa kiasi gani mchezo huo ulikuwa mgumu na vile wachezaji wa Tanzania walipambana uwanjani, walistahili alama moja ambayo ilitosha kuwapeleka Afcon 2023



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz