Taarifa Rasmi kuhusu Majeruhi ya Inonga yalipofikia - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa Rasmi kuhusu Majeruhi ya Inonga yalipofikia

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Beki wa Simba Hennock Inonga amepewa mapumziko ili kuuguza jeraha alilopata katika mchezo dhidi ya Coastal Union


Mchezo huo uliomalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-0, ulipigwa uwanja wa Uhuru jana mshambuliaji wa Coastal Union Hija Ugando akipewa kadi nyekundu kutokana na rfu mbaya aliyomchezea Inonga


Simba imethibitisha kuwa Inonga hakuvunjika na alitarajiwa kuruhusiwa kutoka Hospitalini jana baada ya kutibiwa


Ugando amemuomba radhi Inonga kutokana na tukio la rafu aliyomchezea


"Namuomba radhi Henock kwa maumivu niliyomsababishia haikuwa dhamira yangu kumuumiza. Lengo langu ilikuwa kuwahi mpira lakini lilikuwa ni tukio la haraka na yeye kuwahi kucheza mpira na mimi kumgonga kwenye ugoko"


"Halikuwa tukio zuri na limesababisha madhara hivyo nimuombe tena radhi," alisema Hija baada ya mchezo



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz