Taarifa kutoka Yanga ni kuhusu majeruhi ya Lomalisa - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa kutoka Yanga ni kuhusu majeruhi ya Lomalisa

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mlinzi wa kushoto wa Yanga Joyce Lomalisa Mutambala anatarajiwa kuwa nje kwa wiki moja baada ya kupata majeraha kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc


Mchezo huo uliopigwa uwanja wa Azam Complex jana Jumatano, ulimalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0


Lomalisa alishindwa kuendelea na mchezo huo kwenye kipindi cha pili baada ya kuchezewa rafu mbaya na Hashim Manyanya wa Namungo Fc


Ilikuwa rafu ambayo pengine ilistahili mwamuzi Emmanuel Mwandembwa kumuonyesha Manyanya kadi nyekundu lakini hata hivyo alitoa kadi ya njano


Ni wazi Lomalisa huenda akakosa mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi dhidi ya Al Merrikh ambao utapigwa Septemba 30 katika uwanja wa Azam Complex



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz