Simba yaongeza basi la pili safari ya Zambia - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba yaongeza basi la pili safari ya Zambia

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Baada ya basi lililoandaliwa kuwapeleka mashabiki wa Simba Zambia kushuhudia mchezo wa mkondo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Power Dynamos, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema wameongeza basi la pili na tayari wameanza kupokea nauli


"Tumejaza basi la kwanza lakini kwa sasa tunachukua nauli kwa ajili ya mashabiki watakaokwenda Zambia na hivyo tutakuwa na mabasi mawili kwenda huko," alisema Ahmed


Basi la kwanza lenye siti 57 limejaa siku tisa kabla ya safari ambayo inategemewa kuwa Septemba 13 kwa gharama ya Sh200,000


Simba itacheza mchezo wake wa kwanza katika hatua ya kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Power dynamos Septemba 16 katika uwanja wa Levy Mwanawasa Zambia.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz