Simba kupasha misuli na Pan African ikijiandaa na CAFCL - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba kupasha misuli na Pan African ikijiandaa na CAFCL

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ametaka mechi moja ya kirafiki kabla ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Power Dynamos ambao utapigwa Jumapili, Oktoba 1 katika uwanja wa Azam Complex

Simba imerejea mazoezini leo kuendelea na maandalizi ya mchezo huo baada ya mapumziko ya mwishoni mwa wiki

Imeelezwa Simba huenda ikachuana na Pan African katika mchezo ambao utapigwa uwanja wa Mo Simba Arena, siku ya Jumanne, saa 3 asubuhi

Mwishoni mwa wiki hakukuwa na mechi za ligi kuu ya NBC, ligi ikiwa imesimama kwa wiki mbili ambapo Bodi ya ligi imetoa ufafanuzi uwepo wa kalenda ya mechi za kuwania kufuzu michuano ya CHAN inayohusisha wachezaji wa ndani

Hata hivyo hakuna ratiba yoyote iliyotolewa na CAF kuhusu michuano hiyo licha ya TFF kudai kuiandikia barua CAF mapema ili kupata uthibitisho kama ipo au la



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz