Rais wa Yanga atoa tiketi Bure kwa mashabiki wote El Merrikh vs Yanga kesho - EDUSPORTSTZ

Latest

Rais wa Yanga atoa tiketi Bure kwa mashabiki wote El Merrikh vs Yanga kesho


 Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Rais wa Yanga Sc Injinia Hersi Said amewanunulia tiketi mashabiki wote wa timu hiyo waliosafiri na timu Rwanda kwa ajili ya mchezo dhidi ya Al Merreikh


Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi saa 9 Alasiri (saa 10 Tanzania) katika uwanja wa Pele, Kigali Rwnada


Akizungumza na mashabiki hao nje ya uwanja wa Pele zamani Nyamirambo, Hersi amesema ni heshima kubwa kwa Yanga kuwa na mashabiki ambao wako tayari kujitoa kwa timu yao


Pamoja ya kuwashukuru kwa kusafiri kwa wingi, Hersi alisema wote watapatiwa tiketi zao bure ili waweze kushuhudia mchezo huo


"Sitakuwa na fadhila kama mmesafiri umbali mrefu kuifuata timu kisha mkalipa viingilio, namuagiza Mfikirwa kulisimamia zoezi lenu kuhusu tiketi, hivyo ‘suala la tiketi kesho ondoeni shaka" alisema Hersi


Kiingilio cha chini katika mchezo huo ni Tsh 21,000/-. VIP ni Tsh 104,000/-, Daraja la kati ni Tsh 52,000/- na Kawaida ni Tsh 21,000/-



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz