Afisa habari wa Yanga aanza Tambo mapema tu - EDUSPORTSTZ

Latest

Afisa habari wa Yanga aanza Tambo mapema tu

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe ametamba kuwa moto waliouwasha kwenye ligi kuu ya NBC msimu huu hawatauzima, wataendelea kugawa dozi kwa kila timu inayokuja mbele yao


Baada ya kukamilika raundi mbili za mwanzo, Yanga imejikita kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na alama sita sawa na Azam Fc na Simba lakini Wananchi wana utajiri mkubwa wa mabao ya kufunga


Wakati Azam Fc wakifunga mabao saba na kuruhusu bao 1, Simba wamefunga mabao sita na kuruhusu mabao mawili huku Wananchi wakifunga mabao 10 pasipo kuruhusu bao lolote


Kamwe amesema wamepania kuweka rekodi ya aina yake baada ya mechi 10


"Hii kasi tuliyoanza nayo haitapoa, tunataka baada ya mechi 10 tuwe na mabao 50 na alama 30,"alitamba Kamwe


Yanga ilianza kutetea ubingwa wake kwa kuibamiza KMC mabao 5-0, kisha JKT Tanzania wakafuatia kukumbana na kipigo cha mabao 5-0 pia


Katika mechi nane zitakazofuatia, mchezo dhidi ya Simba ni miongoni ukitarajiwa kupigwa Novemba 05 katika uwanja wa Benjamin Mkapa


Wakati mchezo dhidi ya Namungo Fc ukiwa bado haujapangiwa tarehe, mchezo utakaofauata kwa Yanga ni dhidi ya Ihefu Fc, utapigwa Oktoba 04 uwanja wa Highland Estates mkoani Mbeya


Huu utakuwa mchezo wa kisasi kwa Yanga kwani Ihefu Fc ilichafua rekodi ya Wananchi kutopoteza mechi kwenye ligi msimu uliopita


Wananchi walikuwa wamecheza mechi 49 pasipo kupoteza lakini wakapoteza mechi ya 50 kwa kufungwa mabao 2-1 na Ihefu Fc



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz