Taarifa Mpya kutoka Yanga ni kuhusu mechi za klabu Bingwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa Mpya kutoka Yanga ni kuhusu mechi za klabu Bingwa

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Mchezo wa kwanza wa hatua ya awali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Asas Fc ya Djibout dhidi ya Yanga utapigwa Jumapili August 20 katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi


Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema wamepokea maelekezo kutoka Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kuwa mechi zote za hatua ya awali dhidi ya Asas Fc zitapigwa uwanja wa Azam Complex


Mchezo wa kwanza utapigwa Jumapili ijayo na mchezo wa pili utapigwa Jumapili ya wiki itakayofuata, August 28 katika uwanja wa Azam Complex


Kamwe ametangaza viingilio vya mchezo huo kuwa VIP A 30,000/-, VIP B 20,000/- na Mzunguuko 5,000/-


Kamwe amewataka mashabiki wa Yanga kununua tiketi mapema kwa kufahamu idadi ya mashabiki ambao wanaruhusiwa kuingia uwanja wa Azam Complex



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz