Simba yakusanya Mamilioni mnada kibegi - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba yakusanya Mamilioni mnada kibegi

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Klabu ya Simba jana iliendesha mnada wa 'kibegi' ambapo fedha zilizopatikana zinakwenda kusaidia wodi za Mama na Mtoto kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Zanzibar


Katika mnada huo, jezi ya kwanza kunadiwa iliikuwa ya Rais w Heshima wa Klabu ya Simba, Mohamed Dewji ambayo ilinunuliwa kwa shilingi milioni mbili (2,000,000). Mnunuzi ni Bukara Romario, wauzaji wa vifaa vya michezo

Jezi ya Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson ilinunuliwa kwa shilingi milioni 2.5 na Tawi la Simba Makini


Jezi ya Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango ilinunuliwa na Sandaland kwa dau la shilingi milioni tatu (3,000,000)


Jezi ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ikanunuliwa kwa shilingi milioni nne (4,000,000) na ES & Sons


Jezi ya Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi ikanunuliwa kwa shilingi milioni tano (5,000,000)


Jezi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ikanunuliwa na Benki ya CRDB kwa shilingi milioni 10 (10,000,000) huku kibegi kikinuliwa kwa Tsh Milioni 2.5 na Saleh Majapa


Katika mnada huo Simba imekusanya takribani Tsh Milioni 29



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz