Simba vs Power Dynamos, Yanga vs El Merrikh Ligi ya Mabingwa Afrika - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba vs Power Dynamos, Yanga vs El Merrikh Ligi ya Mabingwa Afrika

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mabingwa wa Zambia Power Dynamos watachuana na Simba katika mchezo wa raundi ya kwanza ligi ya mabingwa barani Afrika


Ni baada ya Power Dynamos kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya African Stars jana na hivyo kufuzu raundi ya kwanza kwa faida ya bao la ugenini baada ya kuchapwa mabao 2-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza


Mchezo wa kwanza utapigwa Septemba 15 huko Zambia na mchezo wa marudiano kupigwa Septemba 29 jijini Dar es salaam


Simba na Power Dynamos zilichuana kwenye Tamasha la Simba Day, Wekundu wa Msimbazi wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa


Timu hizo zinakutana tena mara mbili kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi


Wakati Simba ikichuana na Power Dynamos, Watani zao Yanga wao watachuana na El Merrikh ya Sudan


Jana Yanga ilitinga raundi ya kwanza kwa ushindi wa jumla wa mabao 7-1 dhidi ya Asas Fc ya Djibout wakati El Merrikh walifuzu kwa faida ya bao la ugenini baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana dhidi ya Otoho ya Congo Brazaville


Simba na Yanga zote zitaanzia ugenini katika mechi za kwanza na kumalizia nyumbani mechi zao za marudiano



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz