Mechi ya Yanga vs Azam Fc yaanza kuzua Mapya - EDUSPORTSTZ

Latest

Mechi ya Yanga vs Azam Fc yaanza kuzua Mapya

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuhitimisha ratiba yake ya pre-season  mwishoni wiki kabla kuelekea mkoani Tanga kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Azam Fc


Mchezo huo utapigwa Jumatano, August 09 katika uwanja wa Mkwakwani


Yanga inatarajiwa kuhitimisha pre-season kwa mchezo mmoja wa kirafiki ambao utapigwa Avic Town


Awali mabingwa hao wa Tanzania Bara walikuwa na ratiba ya kucheza mechi moja ya kirafiki uwanja wa Azam Complex, hata hivyo mpango huo hautakuwepo baada ya mapendekezo ya Kocha Miguel Gamondi


Gamondi hayuko tayari vijana wake wacheze mechi ikarushwa mbashara kabla ya Ngao ya Jamii kwani kufanya hivyo ni kuwaonyesha wapinzani wake silaha


Gamondi anataka kuwasurprise wapinzani wake kwa kuwashushia kikosi na mbinu ambazo hawakuzifahamu kabla


Hata Azam Fc ambao wana ratiba ya kuchuana na Bandari Fc Jumamosi katika uwanja wa Azam Complex, awali mchezo huo ulitangazwa kuwa ungeonyeshwa mbashara na Azam TV, lakini kulingana na taarifa iliyotolewa na Azam Fc, hautaonyeshwa na pia mashabiki hawataruhusiwa


Yanga inatarajiwa kuelekea jijini Tanga siku ya Jumatatu tayari kuwakabili Azam Fc siku ya Jumatano



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz