Maxi ni toleo jipya la Mayele - Shungu - EDUSPORTSTZ

Latest

Maxi ni toleo jipya la Mayele - Shungu

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Katika msimu wa 2020/21 Ligi Kuu ya DR Congo, aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele aliitumikia AS Vita na kumaliza katika nafasi ya pili katika mbio za ufungaji bora akifunga mabao 14 nyuma ya Jean Baleke wa Simba aliyefunga mabao 15


Katika tuzo ya mchezaji bora wa msimu huo (MVP), likachomoza jina la Maxi Mpia Nzengeli aliyekuwa akiitumikia AS Maniema Union wakati huo akiwa na umri wa miaka 21 tu


Msimu uliopita Rais wa Yanga Injinia Hersi Said alifanya jitihada kumsajili Maxi lakini haikuwa rahisi AS Maniema kumuachia nahodha wao huyo. Hersi hakukata tamaa, msimu huu akajaribu tena na hatimaye amefanikiwa kumleta Maxi ndani ya klabu ya Yanga


Kocha wa AS Vita Raul Shungu ambaye amewahi kuifundisha Yanga mwaka 1998, amesifu usajili wa mchezaji huyo akiwahakikishia mashabiki wa Yanga kuwa watarajie mambo makubwa kutoka kwake


"Nimeona Yanga wamemsajili Maxi, huyu ni mchezaji mwingine bora kabisa amekuja hapa Tanzania, naweza kusema kama ni kitabu basi Maxi ni toleo jipya badala ya Fiston (Mayele),” alisema Shungu ambaye kikosi chake kiko Tanzania kikifanya pre-season


"Nilizungumza wakati ule Mayele anafika hapa tena kabla ya kuanza kucheza. Nilisema ni mchezaji bora ambaye kama ataweka juhudi atasumbua sana na ikawa hivyo, nafikiri mliona wote sasa vilevile timu pinzani zimchunge huyu Maxi” 


"Kipaji chake ni kikubwa sana anaweza kucheza nafasi nyingi uwanjani, ana nguvu, kasi na kitu kizuri zaidi kwa Yanga watafaidi kwa kuwa ni kijana mdogo atawasaidia sana mtamuona pia akifunga sana," Shungu alinukuliwa na gazeti la Mwanaspoti


Ukweli wa maneno ya Shungu ulianza kuonekana kwenye mchezo wa wiki ya Mwananchi dhidi ya Kaizer Chiefs, Maxi akicheza kwa dakika 45 ambazo zilitosha kumtambulisha kwenye soka la Tanzania



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz