kocha wa viungo wa Yanga aibukia Orlando Pirates - EDUSPORTSTZ

Latest

kocha wa viungo wa Yanga aibukia Orlando Pirates

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Aliyewahi kuwa kocha wa viungo wa Yanga Helmy Gueldich amejiunga na timu ya Orlando Pirates inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini


Helmey alikuwa sehemu ya benchi la ufundi la Yanga lililoshinda mataji sita katika misimu miwili mfululizo likiongozwa na Nasreddine Nabi


Aliondoka Yanga baada ya mkataba wake kumalizika mwishoni mwa msimu uliopita. Awali alikuwa kwenye mpango wa kutua Kaizer Chiefs na Nabi


Hata hivyo mpango huo haukufanikiwa, Nabi amejiunga na FAR Rabat, mabingwa wa Ligi Kuu ya Morocco na Helmey sasa ametua Orlando ambao ni wapinzani wa Kaizer Chiefs


Mafanikio ya Yanga katika michuano ya Kimataifa msimu uliopita yamewapa ulaji waliokuwa makocha katika benchi la ufundi


Aliyekuwa Kocha Msaidizi Cedric Kaze yeye ni kocha mkuu wa Namungo Fc wakati aliyekuwa Kocha wa magolikipa Milton Nienov amerejea kwao Brazil sasa akiwa kocha mkuu wa moja ya klabu inayoshiriki Serie B nchini humo



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz