ILE SHOO YA SIMBA DAY NDO LEO SIKU KUU YA WANASIMBA - EDUSPORTSTZ

Latest

ILE SHOO YA SIMBA DAY NDO LEO SIKU KUU YA WANASIMBA

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 mashabiki wa Simba wakielekea uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya tukio kubwa la Kitaifa


Kwa Wanasimba, Simba Day ni kama sikukukuu, shughuli nyingine zote husimama ili kufurahia siku hii maalum


Simba Day leo itakuwa na ugeni mkubwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Samia Suluhu Hassan atakuwa mgeni rasmi wa tukio hili


Mageti ya uwanja wa Benjamin Mkapa yatafunguliwa mapema tu ili kuwaruhusu mashabiki kuingia uwanjani kwa utaratibu mzuri


Tiketi zote zilishauzwa siku tatu zilizopita, Jeshi la Polisi limetahadharisha kama huna tiketi usiende uwanjani, baki nyumbani fuatilia kupitia Azam TV


Kutakuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wakiongozwa na Ali Kiba, Tunda Man, Joh Makini, Meja Kunta na wengine kibao


Mechi za kirafiki kutoka timu ya Wanawake, timu ya vijana, wakongwe na matukio mengine ya kuwaburudisha Wanasimba


Simba Day leo itahitimishwa na matukio makubwa mawili; la kwanza ni utambulisho wa kikosi cha Simba cha msimu wa 2023/24


Ile shauku kubwa ya kumjua mlinda lango mpya aliyesajiliwa na Simba basi majibu yake ya majira yatapatikana saa 11 jioni


Pili kutakuwa na mchezo wa Kimataifa wa kirafiki kati ya Simba dhidi ya Power Dynamos, mabingwa wa Ligi Kuu ya Zambia

Tukio hili lipo mubashara kwenye app yetu kama hujaipakua bofya hapa kuipakua Bure kabisa



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz