Yanga watangaza mwingine - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga watangaza mwingine

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Uongozi wa klabu ya Yanga jana ulimtangaza Charles Haalubono raia wa Zambia kuwa Kocha Mkuu wa Yanga Princess


Msimu uliopita Yanga Princess haikufikia malengo yake licha ya uwekezaji mkubwa uliofanywa kwenye kikosi


Kuelekea msimu ujao, maboresho yameanza na benchi la ufundi kwani Haaulobono ni kocha mwenye uzoefu mkubwa katika kufundisha soka la Wanawake


Ameinoa klabu ya Green Buffalos ya Zambia kwa miaka 15 akiongoza timu hiyo ya Wanawake kutwaa ubingwa wa ligi kuu mara 6 na taji la CECAFA


Haalubono pia ndiye Kocha wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Zambia umri chini ya miaka 20


Makamu wa Rais wa Yanga Arafat Haji ambaye ni mlezi wa Yanga Princess alitoa ahadi kuwa watafanya maboresho zaidi kuelekea msimu ujao


"Msimu uliopita haukuwa mzuri licha maboresho makubwa tuliyofanya, sasa tunautumia kama changamoto, tutaimarisha mapungufu yote ili kuhakikisha msimu ujao Yanga Princess inatimiza malengo ya kutwaa ubingwa," alisema



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz