Maboresho Benjamin Mkapa kugharimu Tsh Bilioni 30 - EDUSPORTSTZ

Latest

Maboresho Benjamin Mkapa kugharimu Tsh Bilioni 30

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo, Saidi Yakubu amesema serikali imedhamiria kufanya ukarabati mkubwa katika Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam ili kuufanya uwanja huo kuwa wa kisasa zaidi.


Yakubu amesema maboresho hayo yatafanyika katika maeneo ya kuchezea, vyumba vya wachezaji na kutoa viti vyote vya uwanja huo


Yakubu ametoa kauli hiyo leo Julai 27, 2023 Dar es Salaam katika hafla ya utiaji saini na Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) kwa ajili ukarabati huo


Aidha Katibu Mkuu amesema uwanja huo utaendelea kutumika kama kawaida hadi pale ukarabati wa eneo la kuchezea utakapoanza.


Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) liliagiza uwanja huo kufanyiwa maboresho baada ya ukaguzi uliofanyika mwezi May 2023


Uwanja huo unatarajiwa kutumika kwenye michuano ya African Footbal League ambapo klabu ya Simba kutoka Tanzania ni miongoni mwa timu nane zitakazoshiriki


Uwanja wa Mkapa ulizindulwa rasmi mwaka (2007), Mpaka kukamilika uligharimu kiasi cha Tsh Bilioni 137



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz