Huyu hapa mrithi wa Mayele, ni hatari - EDUSPORTSTZ

Latest

Huyu hapa mrithi wa Mayele, ni hatari

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Yanga itakamilisha usajili kwa wachezaji wawili, mmoja wa kigeni na mwingine ni mchezaji wa ndani


Wiki hii Yanga itafunga hesabu zake za usajili kwani dirisha la usajili kwa michuano ya CAF litafungwa Jumatatu ijayo


Baada ya Fiston Mayele kuuzwa, Wananchi wanasubiri kwa hamu ujio wa mshambuliaji atakayechukua nafasi yake


Usajili wa mshambuliaji huyo imeelezwa uko katika hatua za mwisho, Wananchi wakae tayari kumpokea


Hapa tunamzungumzia mfungaji bora wa ligi kuu ya Cameroon 2022/23 Emmanuel Dikongue Mahop kutoka klabu ya Cannon Younde akimaliza msimu na mabao 15, assist 3


Kwa kuzingatia mahitaji ya Yanga msimu ujao, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amepambana kwelikweli kuinasa saini ya mshambuliaji huyo ambaye timu nyingi zimehitaji huduma yake


Mahop ana kasi, nguvu na maarifa ya kuwatoka mabeki. Anatumia vyema miguu yake yote miwili akiwa miongoni mwa washambuliaji wa timu ya Taifa ya Cameroon (sio ile ya CHAN)


Kabla ya kutua Cannone Younde, Mahop aliitumikia Fc Akonagui ambapo katika msimu wa 2019/20 alipachika mabao 24 na kutoa assist 5


Huyu ni mchezaji sahihi kuvaa viatu vya Mayele anayesubiri kutangazwa na klabu ya Pyramids Fc ya Misri



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz