Edo Kumwembe awachana wanaosema Yanga iliweka kiingilio kikubwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Edo Kumwembe awachana wanaosema Yanga iliweka kiingilio kikubwa

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mchambuzi nguli wa masuala ya soka nchini, Edo Kumwembe amewaponda baadhi ya wachambuzi na mashabiki wa soka ambao wamesema chanzo cha Yanga SC kushindwa kuujaza Uwanja wa Mkapa katika Tamasha lao Siku ya Mwananchi ni kiingilio cha Tsh 10,000 kuwa kikubwa.


Tamasha hilo lilifanyika Jumamosi iliyopita ambapo Yanga walitangaza wachezaji wao watakaokuwa nao kuelekea msimu mpya huku wakicheza mechi ya kirafiki na kaizer Chiefs ya Afrika Kuzini ambapo yanga walishinda kwa bao 1-0.


Akizungumzia hilo, Edo amesema; "Umekaa na mtu baa, amekunywa bia 21, ubavu wa mbuzi na kaita demu wake. Bado na yeye analalamika kwamba 'Elfu kumi nyingi kuingia uwanjani'. Yes kuna watu elfu kumi nyingi sana lakini kuna watu wanaiga tu kusema elfu kumi nyingi kwa sababu hawajazoea kulipa au hawajazoea ughali wa mpira.


"Kuna kundi kubwa la wenye uwezo wa kulipa elfu kumi hawaendi uwanjani wakitumia kisingizio cha sh elfu kumi wakati ni wababe wa starehe sehemu nyingine. Tanzania ni miongoni mwa nchi chache ambazo mpira kulipia ni bei rahisi. Yaani anakuja Mahrez unamtazama kwa dola moja tu (sh elfu tatu).


"Kamuulize Injiani aliteseka kumpata Max, Skudu, na wengineo kwa sh ngapi. Hadi dirisha lifungwe ukute wametumia sh milioni 600 kusajili, achana kuvunja mikataba. Simba imetumia sh ngapi kusajili? Kuweka kambi Uturuki? Hata hivyo tunataka kiingilio kiwe dola moja tu kwa ajili ya kufurahisha mashabiki.


"Tumekaa tunasubiri akina Miquissone tuwaone kwa dola moja tu wakati timu imetumia sh milioni 200 kumrudisha nchini. Yeye peke yake achilia mbali akina Onana. Starehe nyingine tunazifanya kwa bei ghali lakini mpira tunautaka uwe rahisi sana. Nchi ya kijamaa sio?," amesema Edo Kumwembe.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz