Chama awatumia salami wapinzani wa Simba, afunguka haya - EDUSPORTSTZ

Latest

Chama awatumia salami wapinzani wa Simba, afunguka haya

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema mchezo dhidi ya Kaizer Chiefs umempa taswira nzuri ya aina ya kikosi alichonacho

Aidha Gamondi ameeleza kuridhishwa na ari, morali na upambanaji wa wachezaji wake huku akiwamwagia sifa kwa kuonyesha kiwango kizuri

"Nawapongeza wachezaji wangu kwa kuwa na mchezo mzuri leo. Tulitawala mchezo na tulitengeneza nafasi nyingi pengine tungeweza kufunga mabao zaidi"

"Nikuhakikishie tuna wachezaji bora na zaidi wako wengine wamenishtua kwa viwango vyao, tuna timu ya kuendelea kuipigania Yanga kupata mataji zaidi"

"Nimewaambia wachezaji tunachotakiwa ni kujiandaa timu ishinde kila mechi ndio maana tupo hapa na hatua hiyo inaanzia sasa hadi mwisho wa msimu, mashabiki wetu wanahitaji kutuona tunavuja jasho jingi kwa ajili ya timu hii kubwa," alisema Gamondi

Gamondi amekiandaa kikosi chake kwa takribani wiki moja tu kabla ya mchezo huo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0

Jambo lililowafurashisha mashabiki wa Yanga ni kuona aina ya uchezaji wa timu yao haujabadilika zaidi yapo maboresho yameongezeka hasa timu inapokwenda kushambulia, kasi inaongezeka 



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

NO COMMENTS:

POST A COMMENT

 Kiungo wa Simba Clatous Chama amesema maboresho yaliyofanyika kwenye kikosi cha Simba, yanampa matumaini kuwa msimu ujao watakuwa na nyakati nzuri


Baada ya kufanya mazoezi kwa siku chache na wenzake katika pre-season huko Uturuki, Chama amekiri kuwa timu imekuwa imara zaidi


"Tupo kwenye maandalizi ya msimu mpya kuna wachezaji wengi wapya tunapambana kuhakikisha tunatengeneza muunganiko mzuri ambao utakuwa na tija ndani ya timu msimu ujao"


"Lengo ni kuhakikisha tunamaliza msimu tukiwa na mataji muhimu ambayo yataturejesha kwenye ushindani hasa kimataifa ambapo tunatamani kuvuka hatua ambazo tayari tumezipiga kwa misimu minne mfululizo hilo linawezekana tukiendeleza juhudi zetu na kuwa wamoja," Chama aliongeza


"Timu yetu imeimarika, wachezaji wote waliosajiliwa ni wazuri, nafikiri tutakuwa na nyakati nzuri sana msimu ujao," alisema Chama


Chama alitua Uturuki Alhamisi iliyopita akiwa na Fabrice Ngoma na moja kwa moja kuanza mazoezi na wenzao waliotangulia



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz