AS Vita Club kujipima na Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

AS Vita Club kujipima na Yanga

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 AS Vita Club ya nchini Congo DR imepanga kucheza michezo kadhaa nchini Tanzania kwa ajili ya kujiweka sawa kuelekea msimu ujao.


Miongoni mwa vilabu ambavyo Vita atacheza nao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC, Yanga SC na Azam FC ambapo mechi hiyo imepangwa kuchezwa wiki ijayo.


Kikosi cha AS Vita kipo njiani kuja nchini Tanzania kuweka kambi ya pre-season kwa siku 14 kujiandaa na msimu mpya baada ya ushauri wa kocha wao msaidizi Raul Shungu.


Shungu aliwahi kufanya kazi nchini miaka ya nyuma akiifundisha Yanga kwa mafanikio kwa kutwa ubingwa wa Ligi Kuu Bara.


"Tunakuja Tanzania tutaweka kambi hapo kujiandaa na msimu mpya, tumeona tuje Tanzania hasa hapo Dar es Salaam kuna viwanja vizuri, tutaangalia kama tutapata kucheza mechi na timu za hapo hizi kubwa," amesema Shungu.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz