Nabi: Achacheni na familia yangu, sikuwahi kujadili na Yanga kuongeza mkataba - EDUSPORTSTZ

Latest

Nabi: Achacheni na familia yangu, sikuwahi kujadili na Yanga kuongeza mkataba

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kutoka insta stori ya Kocha @nabinasreddine; "Habari za jioni, Ningependa kufafanua mambo machache. Uamuzi wangu kuhusu mustakabali wangu na Yanga sc ulichukuliwa na kutangazwa klabuni mara baada ya mechi dhidi ya TP Mazembe. Wakati huo, sikuwa na ofa kutoka kwa klabu nyingine yoyote.


"Ripoti kwenye kituo cha redio kwamba mwanangu alikuwa wakala wangu na amekuja kukamilisha mpango huo ni uongo na upuuzi kabisa. Mwanangu ni mwanafunzi na mfuasi wa klabu, na alikuja kusaidia timu na baba yake. Uwepo wake ulikuwa mdogo tu kwa sababu hizi mbili, kusaidia timu na baba yake.


"Pia ningependa kusema kwamba sikuwahi kukaa na klabu kujadili uwezekano wa kuongeza mkataba, kwa sababu klabu tayari ilijua miezi ya nyuma kuhusu uamuzi wangu, Nimehuzunika kama mashabiki wetu walivyohuzunika kuwa kufikia mwisho wa ushirikiano wangu na klabu.


"Kwa kujiheshimu, ningeomba kuachwa na familia yangu na mtoto wangu ambaye hana uhusiano wowote na maamuzi ya taaluma yangu. Asante Nasreddine Nabi."



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz