Kinara wa mabao Rayon atajwa Simba - EDUSPORTSTZ

Latest

Kinara wa mabao Rayon atajwa Simba


Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc wanatajwa kuwa mbioni kukamilisha usajili wa mshambuliaji Leandre Essomba Willy Onana kinara wa mabao ligi kuu ya Rwanda msimu huu


Onana yuko jijini Dar es salaam tangu juzi wakala wake akidokeza kuwepo kwa mazungumzo baina yake na mabosi wa Simba


Straika huyo wa Rayon Sports ndiye kinara mabao kwa msimu wa 2022-23, alitikisa nyavu mara 16 kwenye ligi ya Rwanda


Ikumbukwe Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ametaka michakato yote ya usajili ikamilishwe mwezi huu ili awe na wachezaji wake wote pale timu itakapoingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa 2023/24


Juzi katika mahojiano na chombo kimoja cha habari, Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangungu alisema watasajili wachezaji watano wa kigeni kwa ajili ya kuimarisha maeneo yote yenye mapungufu



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz