Breaking: Ratiba ya Ligi Kuu England 2023/24 yatangazwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Breaking: Ratiba ya Ligi Kuu England 2023/24 yatangazwa


 Ligi kuu ya Uingereza imethibitisha ratiba ya msimu ujao wa 2023/24


Ratiba ya Ligi Kuu nchini England kwa msimu wa 2023/24 imetangazwa rasmi leo Juni 15, 2023


Mabingwa wa England 2022/23 Manchester City wanatarajiwa kuwa timu ya kwanza kushinda Ligi ya England kwa misimu minne mfululizo, huku Arsenal na Manchester United wakiwa miongoni mwa timu zinazotarajia kuleta ushindani mkubwa.


Luton Town inarejea ligi kuu kwa mara ya kwanza tangu ilipoitwa Division One, ikiunganishwa na Burnley na Sheffield United waliopata nafasi ya kuwa klabu zilizopanda daraja na kucheza Ligi Kuu England.


Chelsea na Tottenham Hotspur zikiwa na uongozi mpya kwa upande wa makocha, huku Liverpool wakitafuta kurejea katika ubora wao baada ya msimu wa 2022/23 kutofanya vizuri na kujikuta wanatupwa nje ya nafsi 4 za kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya na sasa watacheza Europa League wakimaliza msimu kwa kushika nafasi ya 5


Msimu unaanza rasmi Ijumaa tarehe 11 Agosti kwa Burnley kuchuana na Mabingwa wa Ligi Kuu Man City, huku nguli wa zamani wa Citizen Vincent Kompany akiikaribisha timu yake ya zamani kwenye dimba la Turf Moor.


Siku inayofuata, Arsenal watakuwa wenyeji wa Nottingham Forest katika mechi ya kwanza ya chakula cha mchana. Mchezo wa kwanza wa Luton atakuwa ugenini dhidi ya Brighton & Hove Albion, na Sheffield United wanaashiria kurudi kwao na mechi ya nyumbani dhidi ya Crystal Palace.


Mchezo wa kwanza wa Chelsea chini ya Mauricio Pochettino utawakutanisha Liverpool kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, huku Man Utd wakiwakaribisha Wolverhampton Wanderers katika mechi ya ufunguzi Jumatatu usiku wa kampeni ya kuanza kwa Ligi Kuu nchini humo.

KUANGALIA RATIBA NZIMA BOFYA HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz