Fei Toto: Sirudishi Pesa mlizonichangia - EDUSPORTSTZ

Latest

Fei Toto: Sirudishi Pesa mlizonichangia

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kiungo mpya wa Azam FC, Feisal Salum "Fei Toto" amezima minong'ono iliyokuwa ikiendelea mitandaoni kuhusu michango aliyokuwa akichangiwa kwa lengo la kupata fedha na kwenda kufungua kesi katika Mahakama ya usuluhishi wa Michezo CAS akitaka kuvunja Mkataba na Klabu ya Yanga.


Sakata hilo sasa limekwisha na tayari Kiungo huyo ameuzwa kwa Klabu ya Azam FC na amesaini Mkataba wa Miaka mitatu unaotamatika waka 2026.


Akizungumza wakati akitambulishwa katika Makao Makuu ya Azam FC "Mzizima" Feisal amesema;


"Kwanza nimshukuru Mwenyezi mungu kwa kuniwezesha kulimaliza suala hili, vilevile nimshukuru Mh Rais kwa kulifanya wepesi suala hili hali kadhalika na viongozi wa Yanga"


"Kuhusu michango wengi mitandaoni wamekuwa wakiuliza inakuaje, kwanza napenda kuwashukuru kwa moyo wao lakini niseme tu waliochanga ni wengi na siwezi kuwafahamu kwa sababu pesa zimetoka maeneo tofauti tofauti"


"Ninachoweza kusema ni kuwa sitarudisha pesa kwa kila aliechanga ila nitazipeleka kwa watoto yatima msikitini na kanisani na nafikiri zitakuwa zimekwenda mahala sahihi inshallah" amemaliza Feisal



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz